Gossip


Mkuu wa wilaya ya Iringa Mh Richard Kasesela amepiga Marufuku ukataji wa miti katika wilaya ya Iringa, akizungumza katika mkutano ulio wakutanisha wadau mbali mbali wa mazingira ulioandaliwa na asasi isiyo ya kiserikali ijulikanayo kama LEAT  lengo likiwa ni kuiwezesha jamii na Serikali kushiriki , kujadili na kufanya maamuzi ya pamoja katika usimamizi wa maliasili kupitia mfumo wa ufuatiliaji wa uwajibikaji (UJU).

“Ni marufuku kukata miti katika wilaya yangu na nitoe agizo kwamba hata ukiwa na kibali hakikisha unapata na barua toka katika ofisi ya mkuu wa wilaya kinyume na hapo utakuwa umekiuka taratibu tulizo jiwekea” Amesema Mh kasesela, “ukataji wa miti umekuwa na madhara makubwa sana kwa mfano angalieni Kijiji Mfyome palivyo hivi sasa ni tofauti kabisa na palivyo kuwa miaka ya nyuma ilikuwa nadra sana kuona ardhi ukiwa juu katika eneo lile lakini angalia hivi sasa jinsi palivyo haribika hii yote ni kwakuwa miti inakatwa hovyo”
 aliendelea  Mkuu wa wilaya.

Katika hotuba yake ameweka wazi pia mkakati wa Serikali kuhamisha wote waliojenga katika vyanzo vya maji pia wanao fanya shughuli zozote ambazo si rafiki na vyanzo hivo ikiwemo kufyatua tofari na kulima (Vinyungu) wataondolewa .“Hivi sasa tumeanza zoezi la kukamata tofari zote zilizo katika vyanzo vya maji na hadi sasa tumesha kamata tofari zisizo pungua laki moja na zote zitaenda kujenga madarasa” amesisitiza pia kuwa ni marufuku kufanya shughuli yeyote mita sitini toka kilipo chanzo cha maji na atakae kiuka agizo hilo taratibu za kisheria  zitafata mkondo wake.


Mh Kasesela amependekeza kuwa uanzishwe ufugaji nyuki katika maeneo ambayo hayatumiki “Nadhani katika baadhi ya maeneo tunaweza fanya ufugaji wa nyuki kwanza watakuwa walinzi wa misitu yetu pili watakuwa chanzo cha kipato pia ningependekeza wale nyuki wakubwa” , mkutano huo uliowakutanisha madiwani na wadau toka MBOMIPA , NJUMIKIK na wawakilishi toka Pawaga ,Idodi , Tungamalenga , Iringa mjini , Karenga na maeneo mengine ya Wilaya ya Iringa.

Akimkaribisha Mwenyekiti wa Jumuiya ya utunazaji Maliasili  Bwana Ngola Magosi amesema “ kumekuwa na changamoto kubwa katika utunzaji wa mali asili , vijiji havitoi kipaumbele suala la misitu, viongozi na watendaji kujiusisha na uvunaji haramu wa misitu, ushirikiano mdogo uliopo kati ya jeshi la polisi na suala zima la kusimamia misitu. Haya yote yanafanya kazi iwe ngumu sana”  

Mkutano huo ulijumuisha madiwani, wakuu wa idara wa halmshauri ya Iringa, watendeaji pamoja na jumuia za watunza maliasili. Mkutano umeazimia kuitisha kikao cha viongozi wa ngazi za juu akiwemo Mkuu wa mkoa, wakuu wa wilaya wote, wakurugenzi wa halmashauri pamoja na wenyeviti wa halmashauri Pia mashirika yasiyo ya kiserikali yanayo husika na mali asili.                                                                                                             

                                                  Angalia Video hapa Chini.....



               

Post a Comment

 
Top